Televisheni ya Georgia imeonyesha vurugu ndani ya bunge wakati wa kikao.
Mmoja wa mbunge anayeiunga mkono serikali alionekana akirusha kitabu kuelekea upande walipokuwa wabunge wa upinzani, huku wabunge wengine wakipaaza sauti na kusukumana.
Mswaada huo umepelekea kuongezeka kwa ghasia katika bunge la Georgia ambalo hushuhudia vurugu kila mara.
Maafisa wa usalama wa Georgia walitumia maji, gesi ya kutoa machozi na vilipuzi dhidi ya waandamanaji nje ya bunge, jumanne, na kuongeza msako baada ya wabunge kujadili mswaada huo wa mawakala wa nje ya nchi ambao umetajwa na upinzani pamoja na n chi za magharibi kuwa kandamizi na wenye ushawishi wa Russia.
Polisi wanawazuia watu 63 na polisi sita wamejeruhiwa.
Forum